Brief

Nini tunapaswa kubadilisha ili wakulima wadogowadogo wa Babati wawe na kilimo endelevu na waimarike? Mambo ya kujifunza kutokana na utafiti wa kijamii uliofanyika kwa miaka 10. Muhstasari wa ushahidi kutoka Babati

Muhtasari huu unaonyesha fursa zilizopo ili kufanikisha uzalishaji, lishe, pamoja na kipato kwa wakulima wadogowadogo katika wilaya ya Babati, Tanzania. Maelezo haya yametokana na mfululizo wa majaribio ya kitafiti yaliyofanyika chini ya mradi wa Africa RISING tangu mwaka 2012 ikihusisha majaribio ya rutuba ya udongo, kilimo mseto na tathimini za masuala ya kijamii na kiuchumi.
Kazi hii ilifanyika katika vijiji tofauti vya wilaya ya Babati, Tanzania kama vile Long, Seloto, Sabilo, Gallapo, Qash, Ayamango, Riroda, Hallu, Duru na Endanachan. Mahindi, maharage, mbaazi na viazi mviringo ndio mazao makuu yanayolimwa na wakulima wadogowadogo kwa lengo la kupata chakula na pia kwa biashara huku Babati.